Help Children
Love them
Saidia Watoto

Wednesday, November 21, 2018

Diamond akabidhi rasmi kadi za bima ya Resolution kwa wakazi wa Tandale

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Resolution Insurance, Maryann Mugo akikabidhi kadi za bima ya afya kwa wakazi wa Tandale kwa dada wa msanii Diamond Platinum, Diamond aliahidi kuwapatia wakazi 1000 huduma hiyo ya bima (Na Mpigapicha Wetu) 

Na Mwandishi Wetu
Msanii wa muziki wa kizazi kipya Nasib Abdul, Diamond Platinum ameshakamilisha ahadi yake ya kuwapatia kadi ya huduma ya bima ya afya wananchi wa Tandale.

Diamond aliwahi kutoa ahadi hiyo wakati wa sherehe yake ya kuzaliwa ya kuwa angewapatia kadi hizo wananchi 1000 wa eneo hilo ikiwa ni sehemu ya mchango wake kwao.

Wakazi hao wamepewa msaada huo wa bima ya afya kupitia kampuni ya bima ya Resolution Insurance ambapo Mkurugenzi Mtendaji wake Maryann Mugo alibainisha kuwa huduma hiyo ni kwa ajili ya watu wanne kwenye familia.

Alisema,”sisi tunapenda kuwahudumia wananchi kujipatia huduma nzuri za afya na kwa kile alichokifanya msanii Diamond kuwasaidia wakazi hawa huduma ya bima basi ni fahari kubwa kwetu”.

Alisema, wananchi mzitumie vema kadi hizi kwa kuwa ni mkombozi halisi katika maisha yenu na kama mnavyojua kuwa mkikosa bima ya afya ni hatari kwa maisha yenu.

Kwa upande wake msanii Diamond aliyewakilishwa na dada yake Esma kwenye makabidhiano hayo aliwataka wananchi wa Tandale kutumia vema huduma za bima hiyo na kujiwekea akiba ya fedha ili mwisho wa siku huduma hiyo ya mwaka mmoja ikiisha waweze kujihudumia kama kawaida.

Alisema,”Diamond ameniagiza niwashukuru kwa kumwombea nay eye amewakumbuka kwa kuwaletea huduma bora ya afya kwa njia ya kampuni hii ya bima ya Resolution

Friday, August 3, 2018

Empowering girls narrows sciences gender gap

Girls in the science laboratories 
They can make different one supported 



By Evance Ng’ingo                    
THOUGH a considerable number of women are defying the odds by invading the once male dominated sectors such as engineering, medicine, mechanics and so on, the gender gap in science related works in Tanzania remains worrying.

With all the odds heavily stacked against them, women have to battle male chauvinism, poverty and outdated social and traditional norms for them to make it to the top, especially in rural areas.

In many societies, girls face a lot of hurdles in their educational journeys such as pregnancies, early marriages and above all they are responsible for all the domestic chores, which consumes much of their time at home hence they get little time for studying.

This has seen many girls shunning sciences due to the myth that they need more time and attention and they are difficult to study.

This is besides that fact that the United Nations Sustainable Development Goal number five emphasises the availability of quality education for girls and women at large.

But, girls seem to face a barrage of challenges that hinder them from performing well in science subjects.

The Co-founder of Shule Direct, an Institution that offers technical support through online services to secondary school students, Iku Lazaro, said that it is possible to promote science subjects among girls and there are several factors that may attract female students to tackle science subjects

She said that the family is one of the important factors, adding that members of the family have the ability to plant the seeds for girls to like science subjects.

She said once parents and other relatives convince their children to tackle sciences, demystifying it, then it will make them develop an interest in sciences.  

She said that in families that value educating boys, then it is obvious that male children will be highly encouraged to go for science subjects while girls are deprived of such encouragement.

She added, “In my experience, I discovered that once girls are encouraged and given the necessary support, they perform well in sciences, but due to cultural and traditional norms in some societies, girls find themselves consuming more of their time doing domestic chores unlike boys who will get enough time to study”

“Science subjects unlike others need time and boys get this time, while some girls don’t get it. Through Shule Direct I have observed that girls develop interest and love to study sciences; so it is the matter of enabling them to perform better.”

In order to unravel reality on the ground, Woman Magazine visited several schools in Dar es Salaam and talked to some students on their experiences and expectations when it comes to science subjects.

Temeke Secondary School student, Joana John Joana loved sciences from the time she was a child and her had ambition was to become a medical doctor; when she was in primary school, she used to tell her friends of her dreams.

But, when she enrolled for her secondary education, the dream started to disappear into thin air due to the fact that she made new friends who had a negative perception about science subjects and told her how difficult the subjects were.

She said that she fail to get enough time to attend extra lessons and as a result she found herself shifting her focus to arts subjects as they were not difficult and challenging.

Joana added that at home she is mainly responsible for washing dishes, cooking and other girl-related chores and she does them until late at night, depriving her of enough time to study.

“Science subjects need more time and attention; I find them difficult and I have no option but to study arts and I am learning History, Geography and Language, though I could be doing Physics, Biology and Chemistry. But, I am still in love with sciences,” she said.

Joana still believes that despite time constraints that hinder girls from performing better in sciences, she still warns her friends to be careful with study groups, urging them to stay away from friends that threaten them against science subjects.

According to the Benjamin Mkapa Secondary School Mathematics teacher, Juma, society has a role to play in making girl students develop interest in science subjects.

 He said early preparations start from home, pointing out that his experience revealed that there are some girls who are better in science subjects compared to boys in Forms One and Two.

But as time goes on, some girls lose focus and among the reasons being family.

He said that some students fail to get enough time due to domestic chores, while others are discouraged by relatives and friends.

“Girls are bright and very good in sciences once they are enabled to do study well, this can be done through conducive studying environment where teachers and members of the society support them,” he said, adding, teachers have started helping students by offering advice and there are positive results.

The Minister of Education, Professor Joyce Ndalichako has been encouraging girls to tackle science subjects, and teachers to be creative to cultivate interest in girls for sciences.  

The initiatives have started bearing fruit, and there is light at the end of the tunnel in ensuring gender equality by 2030.

In this year’s National Form Six Examinations results, according to the National Examination Council, girl students shined in science subjects with 98.29 percent compared to boys with 97.12.

The performance reveals that once a girl gets effective support, she will do better.

This has spilled to university level as enrolment at the University of Dar es Salaam, UDSM in the year 2017/18 increased to 30 percent compared to the past three years where it ranged around 16 to 17 per cent.

Carolyne Erakyisima is a successful woman owning an organization known as Apps and Girls that offers science subjects to girls aged between 10 to 19 years and teach them IT technology.

She said, “Among the 2,000 girls I have supported, some managed to get sponsorship to different parts of the world; this gives a picture that when girls get support they deliver.”

Doctor, Esther Mwaikambo was the first woman doctor in Tanzania around 1965 after she was admitted to the Friendship University, Moscow, and in 1969 she completed her medical studies and awarded a degree in medicine.

She said that girls are naturally bright and are able to do better in sciences and added that society should stop any harmful and bad treatment to them; instead they should empower them to conquer the world.

“Once society supports these girls, it is obviously that they will do better. Members of the society, teachers and students should work together in enabling girls to perform better in science subjects,” she said.

Arnold Ndumbaro currently owns an engineering company and employs 12 engineers of which five of them are female. He told this newspaper that during his study at Forodhani Secondary in the late 1980s, girls were doing better in science subjects and even at university and he confessed that girls can be best engineers, doctors and even pilots.

According to the UN Secretary-General AntĆ³nio Guterres, both gender needs to work together in attaining the 2030 goals that insist of gender equality in ensuring no poverty, zero hunger, good health and wellbeing, quality education, and clean water and sanitation.

Also affordable and clean water, decent works and economic growth, industry, innovative and infrastructure, reduced inequality, sustainable cities and communities.

With the light shining for the girl child as stakeholders are joining hands to empower and address hurdles, it is imperative that more concerted efforts are made for the world to achieve SDGs and make it a better place for women.


Monday, July 31, 2017

PiMAK yafungua duka Dar

Mmiliki wa kampuni hiyo, Riza Ergun akiwa na wadau kadhaa waliojitokeza kwenye uzinduzi huo

Wafanyakazi na wageni waliojitokeza siku hiyo ya uzinduzi wa duka



Riza Erguna akikata utepe kuashiria uzinduzi wa duka lake hilo hapa nchini

Na Mwandishi Wetu
KAMPUNI ya kimataifa inayojihusisha na utengenezaji na uuzaji wa vifaa vya mbalimbali vya mapishi kwenye hoteli , PiMAK  imefungua duka hapa nchini lililopo Mnazi Mmoja, Dar es Salaam.


Meneja Mkuu wa kampuni hiyo, Ali Donmez alisema, kampuni hiyo imebainisha soko kubwa la bidhaa zake hapa ambapo imekuwa ikifanya biashara kwa muda mrefu kwa kushirikiana na mawakala, na kwa sasa licha ya kufungua duka hilo lakini bado inaona kuna fursa kubwa zaidi za uwekezaji.

Akizungumzia kuhusiana na bidhaa hizo, alisema kuwa ni bidhaa kwa ajili ya matumizi ya hoteli, migahawa na huduma kubwa za mapishi vikiwamo vya kukatia nyama, kuhokea mikate, kuoshea vyombo, kupikia na huduma nyingine za kihoteli.


Aliongeza kampuni hiyo imeshafanya kazi hapa nchini kwa miaka minne ikishirikiana na mawakala ambapo vifaa hivyo vinatumiwa na hoteli nyingi hapa nchini, huku akiweka wazi kuwa inatoa huduma za utengenezaji wa bidhaa hizo pia.


"Kampuni hii ina miaka 25 na makao yake makuu ni Instabul, Uturuki kwa Tanzania tumekuwapo kwa miaka minne tukifanya biashara kwa kushirikiana na mawakala lakini leo tumefungua (jana) tumefungau duka letu huku tukiwa na lengo na kuja kuanzisha kiwanda cha uundwaji wa vifaa hivi hapa hapa nchini" alisema Donmez.



Pia alisema kuwa kampuni hiyo kwa miaka ya baadae itafungua kiwanda hapa nchini kwa lengo la kurahisha upatikanaji wa bidhaa zake kwenye soko la Afrika Mashariki na Kati na pia kuongeza ajira zaidi kwa watanzania.

Kampuni hiyo kwa sasa inafanya kazi nchi 16 na kwa hapa nchini imeshaajiria wafanyakazi 15 huku ikitoa huduma za ukarabati wa vifaa vya upishi hoteli mbalimbali nchini.
==============================================

Wednesday, May 24, 2017

MKUU WA WILAYA YA UBUNGO AAGIZA KUANZA UJENZI WA MADARASA MANNE NA VYOO VYA SHULE YA SEKONDARI MBURAHATI


Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe Kisare Makori akizungumza wakati wa ziara yake ya kikazi katika shule ya Sekondari Mburahati iliyopo Katika Mtaa wa Barafu, Kata ya Mburahati Jijini Dar es salaam.Leo Jumatano, Mei 24, 2017
Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe Kisare Makori akisikiliza maelezo kuhusu shule ya Sekondari Mburahati mara baada ya kuzuru shuleni hapo.Leo Jumatano, Mei 24, 2017
Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari Mburahati Ndg Bagaya Kashato akielezea changamoto zinazoikabili shule hiyo mbele ya Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe Kisare Makori
Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe Kisare Makori akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuzuru  shule ya Sekondari Mburahati .Leo Jumatano, Mei 24, 2017
Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe Kisare Makori (Kulia) akimsikiliza Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari Mburahati Ndg Bagaya Kashato akitoa maelezo kuhusu  kukwama kwa ujenzi wa madara ya shule ya Sekondari Mburahati mara baada ya kuzuru shuleni hapo, Mwingine ni Katibu Tawala wa Wilaya ya Ubungo Ndg James mkubo.Leo Jumatano, Mei 24, 2017
Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe Kisare Makori akisisitiza jambo wakati wa ukaguzi wa madarasa ya shule ya Sekondari Mburahati



Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe Kisare Makori Leo Jumatano, Mei 24, 2017 ameiagiza Ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo inayoongozwa na Ndg John Lipesi Kayombo kuanza mchakato wa ukamilisho wa ujenzi wa Madarasa manne katika shule ya Sekondari Mburahati iliyopo Katika Mtaa wa Barafu, Kata ya Mburahati Jijini Dar es salaam.
Sambamba na Agizo hilo pia ameagiza kujengwa vyoo vya wanafunzi kutokana na uchache wa vyoo vilivyopo ili kukabiliana na wingi wa wanafunzi.
Mkuu wa Wilaya ametoa agizo hilo wakati wa kikao Cha pamoja kilichofanyika Shuleni hapo kwa kuhudhuriwa na Uongozi wa Shule hiyo, Kamati ya Shule, Uongozi wa serikali ya Mtaa na Afisa Mtendaji wa Kata ya Mburahati.
Mhe Makori alisema kuwa kutokana na ongezeko la wanafunzi wanaojiunga na kidato Cha kwanza Kila mwaka kumekuwa na upungufu mkubwa wa madawati Jambo ambalo linachangia wanafunzi shuleni hapo kuanza kusoma kwa kupokezana hivyo mpango mahususi kukabiliana na changamoto hiyo ni pamoja na kuanza kujenga miundombinu ya kutosha itakayowasaidia wanafunzi kupata elimu bora.
Akizungumzia changamoto ya upungufu wa walimu shuleni hapo Mkuu wa Wilaya alisema kuwa wakati serikali inajiandaa na mkakati wa jumla wa kuikabili changamoto hiyo ni vyema uongozi wa shule kutafuta walimu wa muda ili kupunguza kadhia ya wanafunzi kukosa vipindi kwa sababu ya upungufu wa walimu.
Shule ya Sekondari Mburahati ni shule ya kutwa iliyoanzishwa mwaka 2010 ambapo pamoja na kuwa na wanafunzi wengi ina jumla ya vyumba vya madarasa 9 huku mahitaji yakiwa ni vyumba 25 hivyo kupelekea kuwa na upungufu wa madarasa 16.
Hata hivyo Mkuu wa Wilaya Mhe Makori amesema kuwa pamoja na changamoto nyingi zinazoikabili shule hiyo lakini Manispaa ianze na changamoto za utatuzi wa Uhaba wa Madarasa na upatikanaji wa vyoo vya kisasa.
Akitoa neno la Shukrani kwa niaba ya Walimu wenzake, Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari Mburahati Ndg Bagaya Kashato amempongeza Mkuu wa Wilaya ya Ubungo kwa kazi kubwa anayoifanya ikiwemo utatuzi wa migogoro ya Ardhi na ujenzi wa vyumba vya madarasa katika Wilaya hiyo.
Kashato ametumia nafasi hiyo pia kumuomba Mkuu huyo wa Wilaya kusaidia utatuzi wa changamoto ya Upungufu wa vitabu vya kufundishia masomo ya sanaa kulingana na idadi kubwa ya wanafunzi, Kukamilishwa Mfumo wa gesi katika Maabara ya shule hiyo na ujenzi kwa ajili ya jengo la Utawala.
Imetolewa Na;
Ofisi ya Mkuu wa Wilaya Ubungo

Monday, May 22, 2017

Rambirambi za waliopoteza maisha St Vicent zazidi kutolewa

 Wa kwanza kulia ni mwakilishi wa chama cha wamiliki wauza mafuta rejareja  Kanda ya kaskazini  Deipyen Bameda  (TASDOA ) katikati ni Katibu mkuu  TASDOA Tinno Mmasi akiwa anafafanua jambo mara baada ya kumkabidhi mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo Rambirambi zao za vifo vya wanafunzi 32 wa Lucky Vicent
 Dare salaam Independent School (DIS) Anna Msangi akiwa anakabidhi kiasi cha shilingi milioni tatu kwa mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo ikiwa ni mchango wao kwa wanafunzi wa Lucky Vicent
mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo akifafanua jambo ofisini kwake kabla ajapokea rambirambi hizo

Habari picha na  Woinde Shizza,Arusha

Baadhi ya  Wanasiasa  wametakiwa kuacha  mara moja kuchulia tukio la vifo vya wanafunzi 32 wa Lucky Vicent kama sehemu yao ya kujinufaisha  kisiasa, pamoja na baadhi yao kupotosha jamii kupitia  mitandao ya kijamii .

Hayo yamebainishwa jana  na mkuu wa mkoa wa Arusha  Mrisho Gambo wakati alipokuwa akipokea rambirambi za wanafunzi  32 wa Lucky Vicent,zilizotolewa na chama  cha wamiliki  wauza mafuta rejareja (TASDOA) pamoja  na uongozi wa shule binafsi ya Dare salaam Independent School (DIS) ambapo alisema kuwa anasikitishwa sana na baadhi ya viongozi kuchukulia swala hili kama ni sehemu ya kujijengea umaarufu.


Alisema kuwa swala hili sio tukio la kisiasa bali ni mtihani na changamoto kubwa iliyozikumba familia za wananchi wa Arusha ,hivyo linatakiwa kuheshimika na kuchukuliwa kama ni tatizo kubwa lililowakumba wananchi wa mkoa wa Arusha na Tanzania kwa ujumla kwani kuwapoteza watoto hawa ni jambo  la kusikitisha sana kwani walikuwa wanategemewa kuwa viongozi wa baadae.

“pia napenda kuchukuwa fursa hii kuwashukuru kwa kuleta michango yenu kwa ajili ya wanafunzi hawa 32 ila napenda pia kuwakumbusha kuwa  jumla ya watu wote waliopata tatizo walikuwa 38 lakini kati yao waliokufa ni 35 na  na wingine watatu ni majeruhi hivyo napenda kuwasihi wananchi na mashirika ambayo wanaleta msaada wasiangalie waliopoteza maisha tu bali wawakumbuke na wale majeruhi watatu ambao wapo nje kwa matibabu kwani wao pia ni binadamu”alisema Gambo

Alisema kuwa japo kuwa majeruhi wale waliopelekwa nje kutibiwa wanaudumiwa bure lakini kuna wale watu ambao wameenda nao pamoja ya kuwa wanahudumiwa chakula na malazi lakini kwa binadamu waka waida anatakiwa kujitegemea kwa vitu vidogovidogo hivyo ni vizuri kama watu wanaotoa msaada wata wakumbuka na hawa majeruhi .

Kwa upande wake katibu mku u wa  chama cha wamiliki wauza mafuta rejareja (TASDOA) Tino Mmasi alisema kuwa wao kama wamiliki wawauza mafuta wadogowadogo wameguswa sana na msiba huu na ndio maana walioamua kukaa kama wanachama na kuchanga fedha hizi kiasi cha shilingi millioni saba laki saba  ili ziwafariji wafiwa hawa 35 na pia wameaidi kwend a kujichanga tena  kwa ajili ya kuwachangia majeruhi ambao wapo Marekani

“tumetoa hiki kidogo lakini kwa jinsi  tulivyoguswa tutaenda kuchanga fedha zingine kwa ajili ya majeruhi waliopo marekani na tunapenda kukuaidi mkuu wa mkoa tutakuwa nanyi bega kwa bega hadi majeruhi hawa wote wapone na warudi hapa nchini”alisema  Mmasi

Katika michango hii shule ya  shule binafsi ya Dare salaam Independent School (DIS) ilichanga kiasi cha shilingi  milioni tatu  laki moja na nusu  huku chama cha wamiliki wa uzamafuta rejareja wakiwa wamechangia shilingi milioni saba laki saba  huku wote wakiaidi kwenda kukusanya fedha nyingine kwa ajili ya majeruhi.

Sunday, May 21, 2017

Camara Education Tanzania yaendelea kuwanoa wanafunzi


Afisa Mtendaji Mkuu wa Shirika lisilokuwa la kiserikali linalojishughulisha na uwezeshaji wa elimu kwa njia ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano, Tehama, Julia Pierre-nina akiwaelekeza jambo walimu kutokea shule mbalimbali namna bora ya matumizi ya Tehama, pembeni yake ni Mkuu wa Mauzo na Masoko, Adam Kawa (Picha na Evance Ng’ingo)

Monday, December 12, 2016

Wanawake wajasiriamali 29 nchini wapewa mafunzo na Taasis ya Graca Machel

Mmiliki wa shule ya chekechea na msingi ya Barney, Marina Juma akifurahi baada ya kupewa cheti cha kuhitimu mafunzo ya miezi 10 ya kuwajengea uwezo wa wanawake wa kujiendeleza kiuchumi yaliyoratibiwa na Mfuko wa Graca Machel, kulia ni Meneja mradi wa mfuko huo  Korkor Cudjoe na katikati ni Mwenyekiti wa Wafanyabiashara wanawake nchini, Jacqueline Maleko (Picha na Mpigapicha Wetu)
Na Mwandishi Wetu
WANAWAKE 29, wajasiriamali katika nyanja tofauti tofauti wamehitimu mafunzo ya miezi 10 ya ujasiriamali yaliyoandaliwa na Taasis ya Graca Machel.

 Mafunzo hayo yamehusisha wanawake wajasiriamali kuanzia ngazi ya chini ya kati na wajasiriamali wakubwa.

Akizungumzia kuhusiana na mafunzo hayo, mratibu wa mafunzo hayo, Vida Mndolwa alisema, wajasiriamali hao walikuwa wakisoma kila Alhamis ya mwisho wa mwezi na kuwa wapo wanafunzi ambao waliishia njiani kutokana na sababu mbalimbali.

Alisema kuwa kwa kipindi hicho chote wamefundishwa masuala mbalimbali yahusuyo biashara na kuwa washiriki walikuwa na nafasi ya kujifunza zaidi kwa vitendo pia.

Kwa upande wake mgeni rasmi katika ufungwaji wa mafunzo hayo, Mwenyekiti wa Wafanyabiashara Wanawake nchini (TWCC) Jacqueline Maleko, aliwataka wanawake hao kuwekeza zaidi kwenye mafunzo kama hayo.
Pia aliwataka wanawake kujenga utamaduni wa kufuatilia taarifa kuhusiana na masuala ya fursa za kibiashara ili kuzitumia katika kupanua wigo wa shughuli zao.

Jacqueline alisema kuwa wanawake wengi nchini wanashindwa kusonga mbele kibiashara kwa kuwa wanakosa taarifa ambazo zingetumiwa kuwawezesha kusonga mbele kibiashara.


Alisema kuwa ili kukabiliana na hali hiyo ni wakati mwafaka kwa wanawake kwenda kwenye vituo mbalimbali vya kiuchumi au wizara na kuomba kupewa taarifa kuhusiana na miradi ya kusaidia wanawake.

Alisema kuwa ipo miradi 19 ya kuwaendeleza wanawake na vijana kwa ujumla kiuchumi na kuwa kwa sasa hakuna uwazi wa kutosha kuhusiana na miradi hiyo.

"Ni wakati sasa kwa wanawake nchini kutafuta taarifa zitakazoinua biashara na hii ni hasa katika kupata habari za fursa za kibiashara, waende Baraza la Taifa la Uwezeshaji wananchi kiuchumi kuna mengi yanayohusiana na miradi ya maendeleo yanayoweza kuwasaidia wwao kama wanawake" alisema Jacqueline.